| 29.07.2010 | 15:00 UTC
FSB yapewa nguvu zaidi
Moscow:
Rais wa Urusi Dmitry Medvedev amesaini sheria mpya kwa ajili ya kuliimarisha shirika la upelelezi la nchi hiyo FSB.
Ikulu ya Urusi Kremlin imesema sheria hiyo inarudisha desturi iliyokuwa wakati wa enzi ya Sovieti ya kutoa tahadhari kwa watu inayoamini kuwa wanataka kufanya uhalifu.
Shirika hilo la FSB ambalo limechukua nafasi ya lile lililokuwa wakiti wa Sovieti KGB, sasa linaweza likamuita mtuhumiwa kwa mazungumzo ya tahadhari ili kuzuia jaribio la tendo la uhalifu dhidi ya usalama wa nchi.
Hata hivyo wakosoaji wanasema kuwa sheria hiyo inaweza kutumiwa kutishia uhuru wa waandishi wa habari na makundi ya upinzani na kuhujumu ahadi za rais Medvedev za kuendeleza haki za raia.






